Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania

TLSB Logo TLSB Logo
Tafuta kwenye kwa

Shule

Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania (TLSB) kupitia idara yake ya Huduma za Maktaba imeendelea kufanya programu mbalimbali (outreach programs) kwa jamii zenye lengo la kuhamasisha usomaji na matumizi ya maktaba hasa kwa wanafunzi.

Vilevile imefanya semina za uandishi wa vitabu na machapisho pamoja na semina za ujasiriamali kwa wadau.

Programu hizo zimefanywa na Vitengo mbalimbali vya Idara ya Huduma za Maktaba na Maktaba za Mikoa, Wilaya na Tarafa ambazo ni miongoni mwa mtandao wa TLSB wenye jumla ya Maktaba 43 nchi nzima.